
“Tumekuwa wasanii ambao tunaweza tukaunganisha nchi zetu na sasa hivi tumekuwa na kilio kwamba East Afrika iwe pamoja,” amesema rapper huyo ambaye jina lake halisi ni Joseph Haule.
“Tumeona tukimtumia Profesa J ambaye ni artist ambaye ni mkubwa hapa Tanzania na Jose Chameleone ni artist mkubwa yupo Uganda tunaweza tukatengeneza kitu kinaweza kikawa kina maana kubwa sana kwa wananchi wa Afrika Mashariki,” aliongeza.
Profesa amesema video ya wimbo itafanyika Uganda au Afrika Kusini.